Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Serikali yatangaza kuwapiga jeki wabunifu zana za kilimo

by TNC
February 5, 2026
in Swahili
0
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Wizara ya Kilimo Kuwapa Kipaumbele Wabunifu wa Zana za Kilimo

Dar es Salaam – Wizara ya Kilimo imesema inawatambua na kuwapa kipaumbele wabunifu wa zana za kilimo nchini huku ikisema lengo ni kurahisisha shughuli hiyo muhimu ya kiuchumi.

Wabunifu hao wanaotengeneza zana kama matrekta, mashine za umwagiliaji, mashine za kuvunia mazao, mashine za kupandia, mashine za kuongeza thamani, majembe ya kukokotwa na ng’ombe wametakiwa kutengeneza zana hizo wakizingatia ubora.

Kauli hiyo imetolewa Alhamisi, Februari 5, 2026 na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Umwagiliaji na Zana za Kilimo, Athumani Kilundumya wakati akifunga mkutano wa Kwanza wa Kikanda wa Afrika kuhusu Matumizi Endelevu ya Zana za Kilimo jijini Dar es Salaam.

Kilundumya amesema katika kutambua mchango wao, Wizara imeandaa shindano la ubunifu litakalofanyika sikukuu ya wakulima maarufu Nanenane ambapo washindi watapata zawadi.

Kauli hiyo inakuja wakati Serikali kupitia Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba ikizindua mpango wa taifa wa zana za kilimo awamu ya pili wa miaka kumi kuanzia 2025/26 hadi 2036.

"Kwanza tunaidadi ya watengenezaji wadogo tumeshawatambua na siku ya Nanenane tumeandaa eneo lao maalumu ili waweze kushindana," amesema Mhandisi Kilundumya.

Amesema lengo la Serikali ni kuanzisha vituo maalumu vya zana za kilimo vipatavyo 1,000 nchi nzima. Amesema yote hayo yanafanyika ili asiwepo Mtanzania anayelima ambaye atakuwa na kipato cha chini.

Mkutano huo umekusudiwa kuwa jukwaa la kubadilishana mbinu bora, kukuza ushirikiano wa kikanda, na kuhimiza matumizi endelevu ya zana za kilimo zinazochangia kuongeza tija na kipato kwa wakulima barani Afrika.

Tags: jekiKilimokuwapigaSerikaliwabunifuyatangazaZana
TNC

TNC

Next Post

Four decades on, a major party confronts a new political reality

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company