Monday, April 20, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Museveni apiga kura kijijini kwake, mfumo wa bayometriki unashindwa

by TNC
January 15, 2026
in Swahili
0
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Rais Museveni Apiga Kura, Aungana na EC Kurejea Mfumo wa Kawaida wa Upigaji Kura

Rais Yoweri Museveni amepiga kura katika Kituo cha Shule ya Sekondari iliyoko katika kijiji chake cha asili cha Rwakitura ya Karo nchini Uganda, huku akisema anaunga mkono maelezo ya Tume ya Uchaguzi (EC) kurudi kwenye mfumo wa upigaji kura kawaida ili kuepuka usumbufu kwa wananchi.

Museveni amewasili katika Shule ya Sekondari ya Karo, iliyoko katika Kijiji cha Rwakitura, saa 5:25 asubuhi leo Alhamisi Januari 15, 2026 na kusimama kwenye foleni fupi nyuma ya wapigakura watano kisha kukamilisha upigaji kura ndani ya dakika 12.

"Walikuwa na tatizo la mashine za kuthibitisha wapiga kura. Mashine zinafanya kazi. Lakini mwanzoni hazikukubali alama zangu za vidole, kwa sababu nadhani wakati zilipochukuliwa, pembe ilikuwa tofauti lakini uso wangu ulipopigwa picha, mashine ilinithibitisha," amesema Museveni.

"Baadhi ya watu ndani ya EC hawakutuma taarifa za waendeshaji kwenda kwenye mashine. Wengine, hata hadi asubuhi ya leo, hawakuwa wametuma taarifa zao za kibayometria. Je, hili lilifanyika kwa makusudi? Tutalichunguza," ameongeza.

Alipoulizwa kama atakubali matokeo ya uchaguzi, Museveni alisema: "Huu ni mojawapo ya udanganyifu tunaopaswa kuchunguza ili kujua tatizo lilikuwa nini? Kwa hiyo, hatujui kama ilikuwa ni uzembe au sehemu ya udanganyifu, lakini tutachambua mambo yote kwa kina."

Kiongozi huyo mkongwe wa Uganda amesema amekubali pendekezo la dakika za mwisho la EC la kurejea upigaji kura wa kawaida ili kuepusha kuwarudisha wapigakura nyumbani.

"Nilipouliza asubuhi ya leo, niliambiwa kuwa kufikia saa 4 asubuhi mashine zilikuwa zinafanya kazi katika baadhi ya maeneo na maeneo mengine hazifanyi kazi. EC ilipendekeza tupige kura kwa njia ya kawaida, nami nikakubali kwa sababu isingekuwa rahisi wananchi kurudi nyumbani," amesema.

Amependekeza huenda baadhi ya maofisa walikuwa na hofu kuhusu matumizi ya mashine za kibayometriki, hali iliyosababisha ucheleweshaji na akaonya kuhusu dosari zilizokuwepo katika chaguzi zilizopita ambazo ziliruhusu kura za upinzani kuongezwa kwa njia isiyo halali.

Mwenyekiti wa EC, Simon Byabakama amevielekeza vituo vya kupigia kura kurejea upigaji kura katika mfumo wa kawaida baada ya kushindikana kufanya kazi mashine za kwa njia ya kibayometriki, hali iliyosababisha ucheleweshaji wa zaidi ya saa nne, hasa katika Jiji la Kampala, ambayo ni ngome ya upinzani.

Tags: apigabayometrikikijijiniKurakwakeMfumoMuseveniunashindwa
TNC

TNC

Next Post

Kyela eyes Sh100bn from four crops as farmers assured of market, prices

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company