Thursday, January 15, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Safari ya mwisho ya Jenista itakavyokuwa, kuzikwa Desemba 16

by TNC
December 12, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Mazishi ya Aliyekuwa Mbunge wa Peramiho Jenista Mhagama Yataendelea Desemba 16, 2025

Mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa Jumanne ya Desemba 16, 2025 katika Kijiji cha Ruanda, Mbinga mkoani Ruvuma.

Jenista ambaye amekuwa mbunge wa Peramiho kuanzia mwaka 2005, amefariki dunia Alhamisi, Desemba 11, 2025 jijini Dodoma.

Ratiba ya mazishi yake iliyotolewa na uongozi wa Bunge, inaonesha Ijumaa, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Itega, jijini Dodoma.

Ratiba Kamili ya Mazishi

Jumamosi ya Desemba 13, 2025, mwili wa Jenista utapelekwa Kanisa Katoliki Kiwanja cha Ndege ambapo ibada itafanyika.

Viongozi mbalimbali watahudhuria kanisani wakiwemo Spika wa Bunge, Mussa Zungu, Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba na Makamu wa Rais, Dk Emmanuel Nchimbi.

Baada ya shughuli ya kanisani, mwili wa Jenista utasafirishwa kwenda Songea, Mkoa wa Ruvuma.

Desemba 14, 2025, maombolezo yataendelea nyumbani kwa Jenista, eneo la Makambi, Songea Mjini. Siku hiyo mwili utapelekwa Kanisa Katoliki Matogoro, Songea Mjini ambapo ibada itafanyika na baadaye mwili kurudishwa nyumbani.

Desemba 15, 2025, mwili wa Jenista utapelekwa kwa wapiga kura wake Peramiho ambapo shughuli itafanyika Kanisa Katoliki la Peramiho. Viongozi mbalimbali wanatarajiwa kuwepo akiwemo Zungu, Dk Mwigulu na Dk Nchimbi.

Baadaye mwili utarudishwa nyumbani kwake Peramiho.

Desemba 16, 2025, mwili wa Jenista utapelekwa Kijiji cha Ruanda ambapo utahifadhiwa katika nyumba yake ya milele.

Tags: DesembaitakavyokuwaJenistakuzikwamwishosafari
TNC

TNC

Next Post

Tanzania sued at regional court over week-long internet shutdown

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company