Saturday, March 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Nigeria yajipanga kuwalinda watoto dhidi ya utekaji kuelekea Krismasi

by TNC
December 23, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Serikali ya Niger, Nigeria Yaahidi Ulinzi wa Watoto Dhidi ya Utekaji wa Nyara

Nigeria. Serikali ya Jimbo la Niger nchini Nigeria imeahidi kuwalinda watoto dhidi ya matukio ya utekaji katika kipindi hiki kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka za Krismasi na Mwaka Mpya.

Ahadi hii imetolewa Jumatatu Desemba 22, 2025 wakati serikali ya jimbo hilo ikiwapokea watoto na walimu 130 waliotekwa nyara na kuachiliwa huru baada ya kuwa mateka kwa muda wa mwezi mmoja.

Utekaji wao kutoka shule ya bweni ya Kikatoliki katika jamii ya Papiri, Jimbo la Niger, ni miongoni mwa matukio makubwa ya utekaji katika historia ya Nigeria.

Hakuna mtu au kundi lililodai kuhusika na tukio hilo hadi sasa, lakini wakazi wa eneo hilo wanayalaumu makundi yenye silaha yanayotafuta fidia.

Ongezeko la Matukio ya Utekaji Shuleni

Utekaji nyara shuleni umekuwa ishara ya ukosefu wa usalama katika nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika. Sasa mamlaka zinasema zinaimarisha hatua za kiusalama.

Mratibu wa kitaifa katika Kituo cha Kupambana na Ugaidi cha Nigeria, Adamu Laka amesema wanatekeleza hatua za muda mfupi za ulinzi katika maeneo hatarishi dhidi ya watoto na jamii kwa ujumla.

Amesema wanakishirikiana na serikali za majimbo, viongozi wa kimila na wa kidini, ili kupata suluhisho la kudumu kwa ajili ya usalama.

"Elimu haipaswi kuathiriwa na vurugu. Tutaendelea kufuata sera na operesheni zitakazorejesha imani, kufungua tena shule kwa usalama na kuhakikisha kuwa haki ya kila mtoto wa Nigeria ya kupata elimu katika mazingira salama inalindwa," amesema.

Swali la Fidia Linabaki Bila Jibu

Hata hivyo, maafisa wa serikali hawajaweka wazi iwapo walilipa fedha zilizoombwa na watekaji au la ili kuachiwa watoto hao.

"Sidhani kama ni haki sana kwa mfumo au kwa serikali kuulizwa kama pesa zilitumika au la. Jambo la muhimu zaidi ni kwamba tumewarejesha watu hawa bila madhara," alisema Gavana wa Jimbo la Niger, Mohammed Umar Bago.

"Mambo mengine ni yetu sisi, si yenu. Kwa hiyo jambo la muhimu zaidi ni kwamba tumewapata watoto waliopotea, na namna tulivyofanya hivyo, sisi tunaijua."

Shule hiyo ilisema watoto wengi waliotekwa nyara walikuwa na umri kati ya miaka 10 na 17. Watoto hao sasa wataungana na familia zao kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya.

Tags: DhidiKrismasiKuelekeakuwalindaNigeriautekajiWatotoyajipanga
TNC

TNC

Next Post

Only 20pc of bus passengers using online ticketing

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company