Sunday, December 14, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Dk Nyansaho apata warithi PSSSF, Tanesco

by TNC
December 11, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Rais Samia Amteua Fortunatus Magambo Kuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF

Dar es Salaam – Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Fortunatus Magambo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

Kabla ya uteuzi, Magambo alikuwa Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi katika mfuko huo.

Sambamba na Magambo, Rais Samia pia amemteua Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Taarifa ya uteuzi huo, imetolewa leo, Alhamisi Desemba 11, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bakari Machumu, akirejea taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka.

Uteuzi wa Magambo, unaziba nafasi iliyoachwa wazi na Dk Rhimo Nyansaho ambaye Novemba 10, 2025, aliteuliwa kuwa mbunge na baadaye Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Dk Nyansaho alihudumu katika mfuko huo kuanzia Mei 26, 2025 alipoteuliwa kwa mara ya kwanza, akitokea Benki ya Azania kwa nafasi ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara.

Uteuzi wa Mbossa kuwa Mwenyekiti wa bodi ya Tanesco, anarithi mikoba ya Dk Nyansaho ambaye ndiye aliyekuwa na nafasi hiyo hadi uteuzi mpya unafanyika.

Dk Nyansaho ameiongoza bodi ya shirika hilo, kuanzia Desemba mwaka juzi.

Tags: ApataNyansahoPSSSFTanescowarithi
TNC

TNC

Next Post

University commends High Court division for advancing access to justice

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company