Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Kiongozi wa Mbeya akemea majungu, atoa msimamo

by TNC
December 7, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Meya wa Mbeya Ataka Madiwani Kujenga Umoja na Kuheshimiana

Mbeya – Meya wa Jiji la Mbeya, Dourmohamed Issa, amewataka madiwani kujenga heshima kwa viongozi wa chama na Serikali kwa kuhepuka majungu, mifarakano na kuwa sehemu ya kuijenga halmashauri mpya.

Katika hatua nyingine, ametangaza msamaha kwa wale waliomkosea kwa kufungua ukurasa mpya wa safari ya miaka mitano na kuwahakikisha kutoa ushirikiano.

Issa amesema hayo Desemba 5, 2025, mara baada ya kutangazwa kushika nafasi hiyo kwa awamu ya pili na kuwa miongoni mwa madiwani walioapishwa kwenye kikao cha kwanza cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa City Peack jijini Mbeya.

Kikao hicho kilihusisha madiwani 45 kati ya 55 wa Jimbo la Mbeya Mjini na Uyole sambamba na kufanya uchaguzi wa Meya, Naibu Meya na kamati maalumu za kudumu.

"Baraza hili linapaswa kuwa la mfano. Tulinde heshima za viongozi na wabunge kwa kutambua tuna majimbo mawili. Watatushangaa wakiona tunafarakana badala ya kuwa wamoja katika kuleta chachu ya kuibua miradi mipya yenye mchango kwa halmashauri," amesema.

Katika hatua nyingine, ametumia fursa hiyo kutangaza msamaha kwa wale waliomkosea na wanahisi aliwakosea kumsamehe huku akisisitiza hataki majungu na kwamba anamtegemea Mungu.

"Madiwani wenzangu ambao mmechaguliwa kwenye kamati msiwe chanzo cha kutugawa au kugawanyika. Kama ujapata leo, kesho utapata ni suala la muda. Cha msingi ni kushirikiana ili kuwa na baraza la madiwani la mfano," amesema.

Kufunga Milango ya Majungu

Issa amesema anafunga milango ya kupokea majungu na kuhitaji madiwani kujenga hoja za kuleta maendeleo katika Jimbo la Mbeya Mjini na Uyole.

"Ndugu zangu, kwangu milango ya majungu naifunga. Sitataka kuona diwani mmoja ananiletea hadithi za diwani mwingine, lakini atakayenisema aseme. Mimi namtegemea Mungu," amesema.

Meya amesema umefika wakati madiwani kuheshimiana kwa kuondoa makundi na kutozitwisha mzigo kamati za Chama cha Mapinduzi (CCM), kuwa sehemu ya kukaa kusuluhisha kesi mara kwa mara.

Onyo kwa Madiwani

Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya, Mohamed Aziz, amewaonya madiwani kuondoa tofauti zao na kuwataka kwenda kwa wananchi kusikiliza na kutatua kero zao.

Amesema hatua ya kula kiapo ni kujidhihilisha wanakwenda kushirikiana na halmashauri katika kuleta maendeleo sambamba na kuhakikisha wanawafikia wananchi.

"Madiwani ondoeni tofauti zenu. Nendeni mkaunge mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan. Tumeona na kusikia hotuba yake siku akiongea na wazee, ameonyesha wapi tumetoka na tuendako kwa masuala mapana ya nchi," amesema.

Diwani wa Kata ya Nsalaga, Clement Mwandemba, amesema ni wakati wa kuwatumikia wananchi kwa kuwafikia kuona changamoto hususani kwa kundi la vijana.

"Tumefika hapa kwa kuaminiwa na wananchi. Jukumu letu ni kurejea tena kukaa chini kuzungumza na kujua wapi panahitaji kuwekwa sawa," amesema.

Tags: akemeaatoaKiongozimajunguMbeyaMsimamo
TNC

TNC

Next Post

Global coalition condemns rights abuses in Tanzania, call for independent investigation

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company