Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Prof Silayo na Dk Anders wataka uimarishaji wa uzalishaji wa mbegu bora Afrika

by TNC
December 4, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Mazungumzo ya Kina Kuhusu Mbegu Bora za Miti Yapigwa Banjul, Gambia

Banjul, Gambia. Mazungumzo ya kina kati ya Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Profesa Dos Santos Silayo na Dk Anders Pedersen, mtaalamu maarufu wa jenetiki ya miti na mmoja wa waanzilishi wa Tanzania Tree Seed Agency (TTSA), yamekuwa miongoni mwa matukio muhimu katika siku ya tatu ya kikao cha 25 cha African Forestry and Wildlife Commission (AFWC25), kilichoendelea Desemba 3, 2025, jijini Banjul.

Wawili hao wamekutana kando ya kikao na kujadili mustakabali wa upatikanaji wa mbegu bora za miti ikiwa ni nyenzo muhimu katika juhudi za kupambana na mabadiliko ya tabianchi, kuimarisha misitu ya kibiashara na kuongeza uzalishaji wa malighafi za viwanda.

Akizungumzia safari ya taasisi hiyo, Profesa Silayo amesema TTSA iliyoasisiwa miaka ya 1990 ikijengwa juu ya tafiti na ushauri wa wataalamu, kwa sasa imeimarishwa zaidi kupitia Kitengo cha Uzalishaji Mbegu za Miti TFS, ambacho kinahakikisha upatikanaji wa mbegu zilizothibitishwa kisayansi kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi.

"Mbegu bora ndiyo msingi wa misitu imara. Bila chanzo cha kuaminika, hatuwezi kuwa na misitu inayostahimili tabianchi na magonjwa. Misitu ya kesho inaanza na mbegu nzuri leo, na mbegu hizo zinapatikana TFS," amesema Profesa Silayo akiwahimiza wadau na wawekezaji kununua mbegu bora kutoka kwa wakala huo.

Dk Anders, ambaye amekuwa mshauri wa muda mrefu katika sekta ya mbegu Tanzania na Afrika Mashariki, amesema Afrika iko kwenye nafasi adhimu ya kuongoza dunia katika mageuzi ya misitu endapo itawekeza kikamilifu kwenye ubunifu wa kielimu na vyanzo vya mbegu vilivyoboreshwa.

"Tulipoanzisha TTSA tuliona pengo kubwa la upatikanaji wa mbegu bora. Leo mahitaji yameongezeka zaidi, lakini uwezo wa kuzalisha suluhisho upo, hasa kupitia taasisi kama TFS," amesema.

Mazungumzo hayo yameibua tena umuhimu wa kuwekeza kwenye sayansi ya mbegu bora, jambo ambalo linatajwa kuwa uti wa mgongo wa misitu inayohitajika kukabiliana na changamoto za ardhi, viwanda vya mazao ya misitu na mahitaji mapya ya kimataifa.

Tags: AfrikaAndersBorambeguProfSilayouimarishajiUzalishajiwataka
TNC

TNC

Next Post

Pinda ataka tafiti za sayansi katika sekta ya kilimo

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company