Bwawa la Nyida Kushirikisha Wakulima 1,500 Kuboresha Uzalishaji wa Mpunga
Shinyanga – Mradi wa ujenzi wa bwawa la umwagiliaji la Nyida unakaribia kukamilika, lengo lake kuu ni kuboresha uzalishaji wa mpunga katika eneo hilo.
Bwawa hili litahudumia heka 800 za mashamba, na lengo lake ni kuongeza mavuno ya mpunga kutoka gunia 10 hadi gunia 40 kwa kila heka, jambo ambalo litasaidia wakulima kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi.
Kijiji cha Nyida chenye wakazi 1,500 wa wakulima wa mpunga watapata manufaa ya moja kwa moja kutokana na mradi huu. Mradi una jumla ya gharama ya bilioni 13.6 na unawe mita za ujazo 7,800,000 ambazo zitamwagilia mashamba ya mpunga.
Mbali na manufaa ya kilimo, bwawa hili pia utaweka fursa ya ufugaji wa samaki, jambo ambalo litasaidia kuongeza mapato ya wananchi wa eneo hilo.
Kipaumbele cha mradi huu ni kuboresha usalishaji wa chakula, kukuza uchumi wa jamii na kukabiliana na changamoto za kimazingira.
Ujenzi wa bwawa hili unaendelea kwa kasi na unatarajiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu, kwa manufaa ya jamii ya Nyida na vijiji vya karibu.