Sunday, March 15, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Watu wanne wapoteza maisha kwa kuzama majini

by TNC
January 3, 2026
in Swahili
0
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Watu Wanne Wafariki Kwa Kusombwa na Maji Mbeya, Jeshi la Zimamoto Latoa Onyo

Mbeya – Watu wanne wameripotiwa kufariki dunia baada ya kusombwa na maji jijini Mbeya, huku Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani humo likiwataka wananchi kuchukua tahadhari ya ziada kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Jeshi hilo limewasisitiza wananchi kuweka ulinzi maalum kwa watoto, wazee na wenye ulemavu wakati wa kipindi hiki cha mvua kubwa.

Aidha, Jeshi la Zimamoto limewataka wananchi kuendelea kutoa taarifa za majanga popote yanapotokea ili kuweza kuokoa maisha ya wananchi kwa wakati, huku likihakikisha kuwa liko tayari kutoa huduma wakati wowote.

Januari 2 mwaka huu, Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) ilitangaza uwepo wa mvua kubwa kwa siku 10 zitakazoambatana na ngurumo za radi, na Mbeya ikiwa miongoni mwa mikoa iliyotajwa.

Mrakibu Mwanadamizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya, Malumbo Ngata, amesema hadi sasa watu wanne wamepoteza maisha kwa kusombwa na maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha.

Ngata amesema matukio ya kusombwa na maji yalianza Desemba 25 mwaka jana, huku wanaume watatu wakipoteza maisha, akiwemo mmoja aliyesombwa Januari 2 ambaye bado hajapatikana.

Ameeleza kuwa Jeshi la Zimamoto linaendelea na juhudi za kumtafuta mtu huyo katika mito mbalimbali, pamoja na mwanamke mmoja wa Mtaa wa Makunguru.

"Tunaendelea kumtafuta huyu aliyesombwa na maji, tangu Desemba 25 ni watu wanne waliosombwa kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha. Kuna aliyekutwa pale Mkulu inapojengwa barabara baada ya kudumbukia, mwingine alikuwa mwendesha pikipiki," amesema Ngata.

Kamanda huyo ameongeza kuwa kutokana na hali hiyo, wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari wakati wote, na kufuatilia taarifa za Mamlaka ya Hali ya Hewa juu ya utabiri wa mvua.

Amesema tahadhari hizo ziendane sambamba na ulinzi kwa watoto, wazee na wenye ulemavu kuhakikisha wanakuwa salama, na kutoa taarifa kwa Jeshi la Zimamoto pale inapotokea tatizo kwani huduma zipo wakati wote.

"Tunavyo vifaa vya kisasa kutuwezesha kufika popote, wananchi watoe taarifa inapotokea majanga, lakini kwa kipindi hiki cha mvua wachukue tahadhari na kuwalinda watoto, wazee na wenye ulemavu," amesisitiza Kamanda huyo.

Benson Msuya mkazi wa Sokomatola amesema tukio la mwanamke kusombwa na maji limewashtua wengi, akiomba wazazi na walezi kuzingatia usalama wao na familia kwa ujumla ili kuepuka matukio kama hayo.

Naye Judith Methew amelipongeza Jeshi la Zimamoto kwa uwahi wake kwenye matukio, akiomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano ili kulinda usalama pale inapotokea majanga yoyote.

Tags: kuzamakwaMaishamajiniWannewapotezaWatu
TNC

TNC

Next Post

Arusha kupitia upya sheria ya kudhibiti taka ngumu, kulinda mazingira

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company