Tuesday, December 16, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Tusikubali jeshi kuchafuliwa – Rais

by TNC
December 16, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Rais Samia: JWTZ Lisikubali Kuchafuliwa na Siasa

Dar es Salaam – Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan, amelitaka Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kutokubali kuchafuliwa wala kumuacha au kumlinda mtu yeyote mwenye cheo kikubwa au kidogo kukigeuza chombo hicho kuwa cha mashinikizo ya siasa.

Rais Samia amesema jeshi ni chombo tofauti na siasa, iwe Mwana-CCM, Mwana-Chadema au chama kingine katika Serikali, JWTZ litabaki kwa ajili ya kulinda nchi na wananchi wake.

Alieleza hayo jana Jumatatu, Desemba 15, 2025 akifungua mkutano wa tisa wa Mkuu wa Jeshi (CDF) na makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA), mkoani Tanga.

"Kwa hiyo siasa na chombo (jeshi) hiki ni tofauti, ulinzi imara ndio msingi wa maendeleo na amani ya nchi yetu. Kauli mbiu hii, inaakisi ukweli kwamba hakuna maendeleo bila amani," amesema Rais Samia.

"Sasa jeshi la wananchi likiwa chombo muhimu cha ulinzi wa amani ndani na nje ya nchi, linategemewa kuendeleza usalama na amani ili wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo," ameeleza Rais Samia.

Kutokana na hilo, Mkuu huyo wa nchi, ameitaka JWTZ kuitumia kauli mbiu ya ‘ulinzi imara ndio msingi wa maendeleo na amani ya nchi yetu’ kuimarisha ulinzi na usalama wa Taifa.

Mchango wa Wanawake Katika Jeshi

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema wanawake wanaendelea kuthibitisha uwezo katika maeneo mbalimbali ya kijeshi, ikiwemo fani za urubani, uhandisi na udaktari.

"Kwa muda mrefu jeshi letu, limeendelea kuwa la mfano katika ukanda wa Afrika na duniani, kutokana na weledi, nidhamu na utii. Ili kuendelea kuwa jeshi imara na mfano, muhimu kuwekeza kwenye mafunzo na mazoezi yanayoendeana na matishio ya kisasa na matumizi ya teknolojia mpya," amesema.

"Sambamba na kuwekeza katika mafunzo ya kisasa na mazoezi, ushirikiano na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kudhibiti matisho ya kiusalama yakiwemo ya ugaidi," ameeleza Rais Samia.

Tags: JeshikuchafuliwaRaisTusikubali
TNC

TNC

Next Post

Traders seek to block forest produce rules

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company