Monday, December 15, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Ole Millya atangaza kiama kwa viongozi wauza ardhi Simanjiro

by TNC
December 14, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Naibu Waziri Ole Millya Atangaza Vita Dhidi ya Viongozi Wanaouza Ardhi Simanjiro

Simanjiro – Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Ole Millya, ametangaza kiama kwa viongozi wa vijiji wenye tamaa ya kuuza ardhi.

Ole Millya ambaye pia ni Mbunge wa Simanjiro ameeleza kwamba hawatishi wala kuwaogopesha viongozi wenye tamaa ya kuuza ardhi ya vijiji, ila atahakikisha anapambana na wabadhirifu hao.

Akizungumza kwenye sherehe ya misa ya Diwani wa Kata ya Komolo, Saning’o Somi, ya kumshukuru Mungu na kuomba baraka za uongozi, amesema siku za wauza ardhi Simanjiro zinahesabika.

"Siwatishi ila nitakula sahani moja na wala ardhi Simanjiro ambao baadhi ya viongozi walikuwa wanafiki, kwani midomoni wanapinga uuzaji ila marafiki zao ni wauza ardhi," amesema Ole Millya.

Ameeleza kuwa siku zote za maisha yake atapinga uuzaji wa ardhi holela, akiwa mbunge au asiwe mbunge, kwani ni kilio kikubwa kwa watu wanyonge ambao wanategemea ardhi kwa ajili ya kuendeshea maisha yao.

Naibu Waziri amesema baadhi ya wenye tamaa ya kuuza ardhi huwa wanaopatiwa maeneo ikiwemo ekari 10, anauza kisha anaenda kupewa eneo jingine na kuuza tena.

Viongozi Wamtakia Kila la Heri Diwani Mpya

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Manyara, Peter Toima, amesema kwa mara ya kwanza Wilaya ya Simanjiro imepata kiongozi wa serikali katika ngazi ya Naibu Waziri, hivyo wanashukuru.

Padri Edwin Kiromo wa Kanisa Katoliki Misheni ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili Terrat amemtakia kila la heri Somi kwa kupeleka furaha kwa watu wa Kata ya Komolo.

"Tusiwe na hila wala upendeleo kwani hata Mfalme Suleiman hakuomba mali wala ng’ombe, aliomba hekima akapewa na mali juu. Hivyo tembea na Mungu katika uongozi wako," amesema Padri Kiromo.

Mchungaji Agustino Laizer amemweleza Somi kuwa kiti alichokalia siyo cha starehe wala cha raha, ni kiti cha kutatua matatizo na changamoto za watu wa Kata ya Komolo.

Tags: ardhiAtangazaKiamakwaMillyaOleSimanjiroViongoziWauza
TNC

TNC

Next Post

Wataalamu watoa suluhu ya kudumu kwa tatizo la maji

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company