Thursday, December 11, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Hali ilivyo mitaani leo Siku ya Uhuru

by TNC
December 9, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Watanzania Waadhimisha Uhuru Majumbani Kutokana na Usalama

DAR ES SALAAM – Watanzania mwaka huu wamesherehekea maadhimisho ya miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika wakiwa majumbani pamoja na familia zao, hali ambayo ni tofauti na desturi ya wengi kutumia siku hiyo kupumzika kwenye maeneo ya burudani au kushiriki matukio ya hadharani.

Mabadiliko hayo yalichochewa na taarifa za uwezekano wa maandamano yasiyo na ukomo tarehe hiyo, baada ya maandamano ya Oktoba 29 wakati wa uchaguzi yaliyosababisha vurugu, ambapo watu walipoteza maisha, wengine kujeruhiwa na mali za umma na binafsi kuharibiwa.

Serikali ilitoa agizo la kuwataka wananchi wote wasio na dharura kusalia nyumbani ili kuhakikisha usalama wa umma. Salamu za heri kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan, zilizowasilishwa na Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba, ziliwahimiza Watanzania kutumia siku ya Uhuru kwa kukaa nyumbani na familia zao.

Tangazo la Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, kwamba watu wanaolazimika kutoka nje wabebe vitambulisho na wawe tayari kuulizwa maswali ya uthibitisho, liliongeza umakini na kuwafanya wengi wachague kubaki majumbani. Uwepo wa askari polisi na wanajeshi katika baadhi ya mitaa uliongeza hisia za tahadhari.

Changamoto za Usafiri

Hata hivyo, kwa wale waliolazimika kusafiri kutokana na dharura, hali haikuwa rahisi. Usafiri wa umma ulipungua kwa kiasi kikubwa kutokana na watoa huduma wengi kutii agizo la Serikali, jambo lililowaadhiri watu waliolazimika kwenda hospitali, kazini au kwenye shughuli muhimu.

Upungufu huo ulisababisha baadhi ya madereva wa bajaji na bodaboda kupandisha nauli mara dufu, jambo lililoleta malalamiko kutoka kwa wananchi waliokuwa na dharura.

Hali Nchini

Dar es Salaam: Eneo la Kariakoo makutano ya Barabara ya Lumumba na Mtaa wa Mkunguni kuelekea Barabara ya Bibititi kukiwa hakuna wafanyabiashara wala watu wanaopita asubuhi ya Jumanne Desemba 9, 2025. Mlimani City ambalo limezoeleka kuwa na pilikapilika za magari na watembea kwa miguu liliwa kimya kabisa.

Moshi: Hali ya utulivu imetawala Manispaa ya Moshi, huku maduka mengi yakiwa yamefungwa katika eneo la Soko la Mbuyuni. Kwa kawaida mji wa Moshi huwa na pilikapilika nyingi, lakini mitaa iliyozoeleka kuwa na shughuli za kibiashara imeonekana kuwa katika ukimya.

Kibaha: Mtaa wa Loliondo Manispaa ya Kibaha Mkoa wa Pwani maduka mengi hayakufunguliwa tangu saa kumi na mbili asubuhi hadi saa nne, eneo ambalo kwa kawaida wananchi hufurika kupata mahitaji muhimu.

Mbeya: Hali ya utulivu imetanda katika maeneo ya Soweto, ambapo saa 5:00 asubuhi baadhi ya maduka yamefungwa. Jana Desemba 8, soko hilo lilishuhudia umati wa wananchi wakifanya ununuzi. Huduma ya usafiri ukiwamo bajaji na daladala imekuwa changamoto, huku bodaboda wakionekana kwa nadra.

Mfanyabiashara Suleiman Hashim amesema wananchi walinunua mahitaji siku nyingi kabla ya tarehe 9, hivyo ameamua kufunga biashara. Barabara ya Sam Nujoma pia imeshuhudia utulivu mkubwa.

Segerea: Wafanyabiashara na wasafirishaji wamefunga maduka na kusimamisha huduma za usafiri. Kituo cha Mabasi cha Segerea Mwisho hakikuonekana na mfanyabiashara wala gari la usafiri.

Tandale na Magomeni: Maeneo haya ambayo kwa kawaida yana hekaheka nyingi yamekuwa tulivu. Kuanzia Magomeni Usalama, Kota hadi Tanesco, hakuna maduka wala huduma nyingine zilizofunguliwa. Ukimya umetawala kiasi cha kufananisha mazingira na siku ya msiba.

Abdulrahman Maulid amesema wananchi wametii maelekezo ya Serikali, na wengi walikuwa wamejiandaa mapema kwa kununua mahitaji muhimu. "Safari hii sijaona mtu anayeangaika kutafuta mahitaji, kwa sababu maandalizi yalishafanyika. Kingine mtandao upo, tofauti na Oktoba 29," alisema.

Hata hivyo, baadhi ya maduka yamefunguliwa kwa muda mfupi kutoa huduma kisha kufungwa, huku watu wachache wakionekana mitaani.

Tags: haliIlivyoleoMitaaniSikuUhuru
TNC

TNC

Next Post

Tanzania renews call for investment in high-quality tree seeds to secure future forests

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company