Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Waziri aonya ujenzi wa miradi chini ya kiwango

by TNC
December 4, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Unguja. Waziri wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar, Nadir Abdullatif amesema wizara hiyo haitomvumilia mkandarasi yeyote atakayefanya kazi za ujenzi chini ya kiwango kisichoheshimu mkataba wa makubaliano yao.

Nadir ameyasema hayo Alhamisi Desemba 4, 2025 akiwa kwenye ziara ya kukagua ujenzi wa vituo vya kupokea na kupozea nishati ya umeme vilivyopo kisiwani Unguja.

Amesema, wananchi wana matumaini makubwa na wizara hiyo hivyo haitakuwa tayari kuwaacha makandarasi kujenga miradi chini ya kiwango na ikawafanya wananchi kupoteza imani kwao.

Vilevile, amesema ujenzi wa vituo hivyo unalenga kutatua kero za wananchi kuhusu changamoto ya nishati ya umeme hivyo ujenzi huo utaifungua Zanzibar kupata umeme wa uhakika.

Ameeleza, Serikali imedhamiria kuwa na nishati ya umeme wa uhakika ili kuongeza idadi ya wawekezaji visiwani humo na wafanyabiashara waendelee kuzalisha.

Amesema, kituo cha umeme kilichopo Welezo kitakuwa kituo kikuu cha kupokea umeme utakaotoka Fumba na baadaye kusambazwa katika kituo cha Makunduchi na Matemwe ili kufika kwa wakati bila ya changamoto.

Naibu Waziri wa wizara hiyo, Seif Kombo Pandu amesema mradi huo ni wa kimkakati hivyo kuna kila sababu ya wataalamu wa ujenzi kujenga kwa kiwango kinachoridhisha kwa maendeleo ya wananchi.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Joseph Kilangi amesema mradi huo unajengwa kwa kutumia fedha za mkopo wa Benki ya Dunia na unalenga kuwanufaisha wananchi.

Amesema, kuwepo kwa kituo cha kupozea nishati ya umeme na kupokelea hapa Zanzibar kitaondosha upotevu wa nishati hiyo wakati wa kusafirishwa.

Mshauri wa mradi huo amesema ujenzi umeshafikia asilimia 55 na utakamilika kwa muda uliopangwa.

Tags: AonyachinikiwangomiradiujenziWaziri
TNC

TNC

Next Post

Rising student suicides expose deepening mental health crisis

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company