Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Serikali na wajumbe wa Tume ya Chande wapewa siku saba kuwasilisha utetezi

by TNC
December 3, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Mahakama Kuu Yatoa Maelekezo Kuhusu Shauri la Tume ya Rais

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imeipa Serikali na wajumbe wa Tume ya Rais ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025, wanakabiliwa na shauri mahakamani kuwasilisha utetezi wao.

Pia, mahakama hiyo imewataka waombaji katika shauri hilo la maombi ya kibali cha kupinga uteuzi wa tume hiyo, kuwapatia wajibu maombi, wajumbe wa tume hiyo, nyaraka za shauri hilo ndani ya siku mbili.

Maelekezo hayo yametolewa Jumanne, Desemba 2, 2025 na Jaji Hussein Mtembwa anayesikiliza shauri hilo, wakati lilipotajwa kwa mara ya kwanza.

Tume hiyo inayoongozwa Jaji Mkuu wa Tanzania mstaafu, Mohamed Chande ilizinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan Novemba 20, 2025 kuchunguza matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Wakati shauri hilo lilipotajwa, waombaji hao wamewakilishwa na mawakili, Mpale Mpoki (kiongozi) na Hekima Mwasipu, huku Serikali imewakilishwa na mawakili wake Mark Mulwambo, Stanley Kalokola na TLS ikiwakilishwa na Ferdnand Makore.

Hata hivyo, japo shauri hilo limetajwa kwa njia ya mtandao, mwenyekiti na wajumbe wa tume hiyo ya Rais hawakutokea.

Wakili Mpoki ameieleza mahakama kuwa walikuwa hawajawapatia nyaraka zinazohusiana na shauri hilo wala taarifa ya mahakama ya kuwepo kwa kesi hiyo.

Kwa upande wake Wakili Mulwambo ameiomba mahakama iwape siku 10 kuwasilisha kiapo kinzani kujibu madai hayo.

Hata hivyo, Jaji Mtembwa amewaelekeza waombaji kuwapatia nyaraka na hati ya taarifa ya kesi hiyo wajibu maombi wa pili mpaka wa tisa (mwenyekiti na wajumbe wa tume) na mahakama hiyo imeipa siku saba Serikali na wajibu maombi wengine wote kuwasilisha viapo kinzani.

Hivyo, Jaji Mtembwa amepanga shauri hilo litajwe Desemba 10, 2025, siku ambayo wadaiwa wote watatakiwa kufika mahakamani, kwa ajili ya kuangalia kama maelekezo hayo yametekelezwa kabla ya kutoa amri nyingine.

Katika shauri hilo lililofunguliwa chini ya hati ya dharura, waombaji hao wanaomba kibali kufungua shauri la maombi ya mapitio ya Mahakama kuomba amri za kufuta na zuio la uamuzi wa Rais wa uteuzi wa wajumbe wa tume hiyo.

Wanahoji uhalali wa uteuzi huo, wakidai ulifanywa kwa nia ovu, kinyume cha kanuni hiyo ya haki asili.

Tags: ChandeKuwasilishaSabaSerikaliSikuTumeUteteziWajumbeWapewa
TNC

TNC

Next Post

Muhimu kuyajua matokeo baada ya ghasia za kuangusha Serikali

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company