Monday, December 8, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Sababu za tovuti na programu kushindwa kufanya kazi duniani kote

by TNC
November 19, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Dar es Salaam – Baadhi ya tovuti duniani pamoja na aplikesheni kama X, PayPal na ChatGPT leo Jumanne zimepitia changamoto ya kushindwa kufanya kazi kutokana na hitilafu iliyojitokeza kwenye miundombinu ya intaneti ya kampuni ya Cloudflare.

Cloudflare ni kampuni inayosaidia tovuti kulinda na kudhibiti trafiki ya intaneti. Kazi kuu ya Cloudflare ni kusaidia kulinda na kuharakisha rasilimali za intaneti.

Ilianzishwa mwaka 2009 kwa lengo la kudhibiti barua taka (email spams) lakini imebadilika na leo inahudumia mamilioni ya watumiaji kwa kutumia DNS na huduma za usalama.

Cloudflare leo imesema tatizo lilianzia saa 6:30 asubuhi likisababishwa na faili la mipangilio (setting file), lililotengenezwa ki-otomatiki kwa ajili ya kudhibiti vitisho vya kiusalama.

TNC imeelezwa kuwa faili hilo lilikuwa kubwa kupita kiasi na kusababisha mfumo wa kushughulikia mtiririko wa data kuanguka, jambo lililosababisha huduma kadhaa kushindwa kufanya kazi.

Katika changamoto hiyo baadhi ya watumiaji wameshindwa kufungua tovuti kwani wamekutana na ujumbe wa Cloudflare error.

Ujumbe uliokuwa unajitokeza ukifungua aplikesheni au tovuti mbalimbali ulikuwa unasema "Please unblock challenges.cloudflare.com to proceed". Wengine walipokea jumbe za Error wakati wanapanga mitandaoni.

Kwa sasa mtandao huo umerudi kawaida na watu wanaweza kutumia aplikesheni au tovuti mbalimbali kama kawaida kwani changamoto hiyo iliyojitokeza kuanzia muda wa asubuhi mpaka jioni imetatuliwa.

Cloudflare wamefahamu na wamechunguza suala hilo kwa undani ambalo hakuathiri wateja wengi.

Hata hivyo kampuni hiyo imehakikisha baadhi ya mifumo itaendelea kupata changamoto huku ikijitahidi kutatua matatizo ya kiufundi yanayowakabili.

Changamoto hii inakuja ikiwa ni mwezi mmoja baada ya kukatika kwa huduma za wavuti za Amazon ambapo tovuti na programu zaidi ya 1,000 zilikatika nje ya mtandao.

Mtoa huduma mkuu wa huduma za wavuti, Microsoft Azure, pia aliathiriwa muda mfupi baadaye na tatizo hilo.

Tags: DunianikazikoteKufanyaKushindwaProgramuSababutovuti
TNC

TNC

Next Post

Samia rings the changes with new Cabinet

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company