Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Askofu Nyaisonga ataja mambo sita kuhusu vurugu za Oktoba 29, asisitiza…

by TNC
November 10, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Mbeya. Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu Mbeya, Gervas Nyaisonga amewaongoza waamini na wananchi katika ibada maalumu ya kuwaombea walioathirika kwenye vurugu wakati na baada ya uchaguzi mkuu, huku akitaja malengo sita ya ibada hiyo.

Uchaguzi mkuu ulifanyika Jumatano ya Oktoba 29, 2025 ambapo kuliibuka vurugu katika maeneo mbalimbali nchini na kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali na miundombinu kabla na wakati wa shughuli hiyo.

TNC imeripoti kuwa Jumapili Novemba 9, 2025 katika ibada iliyofanyika Kanisa Mwanjelwa jijini Mbeya, Askofu Nyaisonga amesema wakati na baada ya uchaguzi ilitokea vurugu zilizosababisha mauaji, majeruhi na uharibifu wa mali za umma na binafsi.

Amesema miongoni maeneo yaliyoathirika ni pamoja na Mbeya na Songwe, ndio maana Kanisa hilo kuamua kuwaombea waliopoteza maisha, kujeruhiwa na walioathirika na matukio hayo.

"Madhumuni ya misa hii yapo sita, kuwaombea marehemu, kuwaombea majeruhi, kumuomba Mungu asaidie jitihada kuwapata waliopotea wawe hai au wamekufa, kuwapa pole waliopoteza mali zao, kutoa rai ya kujitathimini na kuomba uponyaji kutoka Mungu wetu," amesema.

"Katika uchaguzi wa mwaka huu kumetokea vifo vya wenye hatia na wasio na hatia, wamo watoto, vijana na wazee, wanawake na wanaume, raia na askari na Novemba 4 nimeshuhudia wingi wa watu waliokuwa wakinunua majeneza, misafara ya magari wakisafirisha vilio kwenda nje ya Mbeya," amesema Nyaisonga.

Askofu huyo amesema kutokana na matukio kuwa mengi kwa wakati mmoja na haijulikani nani apewe pole au nani aachwe, badala yake misa hiyo inatoa pole kwa ujumla kwa waliofikwa na madhila yoyote.

Amesema kabla na wakati wa uchaguzi mkuu, watu kadhaa waliripotiwa kupotea kwa mazingira ya kutatanisha na wasio julikana, akieleza wanaomba Mungu asaidie wapatikane kwa mazingira yoyote.

"Tumeshuhudia upotevu na uharibifu wa mali za umma na binafsi, tunawapa pole kwa hasara mbalimbali, Mungu ameleta hili ili tugutuke kutoka kwenye usingizi uliotusahaulisha mambo ya msingi," amesema.

"Tunatoa mwaliko wa kujitathimini, nchi yetu ilionekanaje wakati moto ukiwaka maeneo mbalimbali…hata mbinguni walishangaa, barabara na madaraja yanajengwa, huduma zinatolewa, lakini unajiuliza kwa nini tufikie hatua hii mbaya," amesema Askofu Nyaisonga.

Amesema, "lakini yote hayo unaweza kusema labda wanaofanya hivi hawaoni mazuri, labda ni maadui, chuki binafsi au wanatoka nje labda labda labda zitakuwa nyingi ila ukitafakari sidhani kama wahuni wanaweza kujitokeza kwa wingi wakati mmoja hata wahuni hawawezi kufa kwa sababu za kijinga."

Amesema lazima kukubali kuwa zipo sababu za msingi hadi kufikia hatua hiyo na kwamba lazima kutafuta wadhamini safi wenye uwelekeo na utayari wa toba, ili kujua kiini cha tatizo hilo na kutoruhusu baadhi ya watu kutumia fursa za machafuko nchini.

"Tunaomba Mungu aliponye Taifa letu na kuliepusha na migogoro na atuponye sote, kwa unyenyekevu niwaombe wafiwa wasamehe na wawe tayari kuanza upya kama wajasiri kujenga upya kwa faida ya waliopo na wajao," amesema Askofu huyo.

Tags: asisitizaAskofuatajaKuhusuMamboNyaisongaOktobaSitavurugu
TNC

TNC

Next Post

Kesi ya Lissu kuendelea kesho baada ya kukwamishwa na uchaguzi

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company