Thursday, October 30, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Kama unaangalia video Instagram ghafla ikakupotea fanya hivi kuiona tena

by TNC
October 26, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Jinsi ya Kuona Tena Video Zilizopotea kwenye Instagram

Dar es Salaam – Watumiaji wa Instagram wanapaswa kufahamu wanaweza kuiona tena ile video ambayo wameipenda ila kwa bahati mbaya imepotea aidha kwa kuji-refresh au kutoka kabisa kwenye timeline ya mtandao huo.

Mfano unaangalia video kisha ukaipenda ila kabla hujaipakua au kushea kwa mwenzio ikapotea na hujui utaipata wapi basi unapaswa kufanya yafuatayo ili kuiona tena.

Kwa sasa mtandao huo wenye watumiaji zaidi ya bilioni mbili kila mwezi na takribani milioni 500 kila siku umekuja na kipengele kipya cha kuiona tena post iliyokupotea.

Ikumbukwe Instagram ni jukwaa la mtandao wa kijamii lililozinduliwa mwaka wa 2010 sasa linamilikiwa na Meta Platforms, Inc., kampuni mama ya Facebook na imekua ikija na masasisho kila wakati ili kuboresha huduma zake.

Hatua za Kuona Tena Video Zilizopotea

Ili kuiona tena video hiyo unatakiwa kwenda kwenye kipengele cha Setting, kisha nenda palipoandikwa ‘Your activity’ shuka chini kisha utaona mahali pameandikwa ‘Watch History’.

Ukifungua watch history utaona video zote ambazo umeziangalia ikiwa ni kwa muda wa siku 30. Hivyo ambayo ilikupotea utaiona hapo.

Vilevile ukiwa katika kipengele hichohicho cha ‘Your activity’ unaweza kuangalia post zote ulizo ‘likes’, comments au reposts, tag.

Katika kipengele hicho cha ‘your activity’ unaweza kuangalia historia yako ya kutafuta vitu kwa kwenda kwenye kipengele cha ‘recent searches’ kisha ukaangalia akaunti ulizotafuta.

Udhibiti wa Muda wa Matumizi

Unaweza kuweka muda wa kuperuzi kama unatumia muda mwingi.

Pia, unaweza kuangalia muda unaotumia kuperuzi kwenye Instagram kwa muda wa juma zima kwa kwenda chini utakuta kipengele kimeandikwa ‘Time spent’ kisha utaona kwa kuanzia Jumatatu umetumia saa ngapi kuperuzi hadi Ijumaa.

Ukiona unatumia muda mrefu kwa siku na unataka kujizuia unaweza kuweka kikomo kwa kushuka chini utakuta sehemu imeandikwa daily limit kisha unachagua utumie Instagram kwa dakika 15 kwa siku, 30, 45, saa moja au mawili.

Ukishaweka muda basi Instagram watakutumia ujumbe wa kufunga mtandao huo wakati unatumia na muda umeshafika.

Tags: fanyaGhaflaHiviikakupoteaInstagramkamakuionatenaunaangaliaVIDEO
TNC

TNC

Next Post

Sh21.9 bilioni kuibadilisha Mpanda

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company