Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Mwandishi wa televisheni na wengine watatu wafutiwa mashitaka ya uhaini na DPP

by TNC
November 26, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Arusha. Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imewaachia huru na kuwafutia mashtaka ya uhaini washtakiwa wanne akiwemo mwandishi wa habari wa Ayo TV, Godfrey Ng’omba.

Wengine walioachiwa ni watoto watatu wa kiume wenye umri wa miaka 13, 16 na 17 ambao kwa pamoja walikuwa wakishtakiwa kwa kesi ya uhaini.

Uamuzi huo umefikiwa Jumanne Novemba 25, 2025 na Hakimu Mkazi Regina Oyier, baada ya Wakili wa Serikali kuieleza mahakama kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi yao chini ya kifungu cha 92(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), sura ya 20 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023.

Washtakiwa hao walikuwa wakishtakiwa na wenzao 59 katika kesi ya uhaini ambapo wanawakilishwa na mawakili kadhaa wakiongozwa na Khamisi Mkindi, mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Arusha.

Washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na makosa ya kula njama ya kutenda kosa kinyume na kifungu cha 384 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu na kutenda kosa lenyewe.

Wanadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Oktoba mosi hadi 29, 2025 walifanya njama mbalimbali za kutenda kosa la uhaini.

Kosa la pili ni kufanya uhaini kinyume na kifungu cha 39 (2) (d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Baada ya maombi hayo, Hakimu Regina amefikia uamuzi wa kuwaachia huru bila masharti yoyote.

Jumatatu Novemba 24, 2025, washtakiwa wengine 24 wa kesi za uhaini mkoani Arusha waliachiwa na mahakama hiyo na kuwa watakuwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha mwaka mmoja wakitakiwa kuripoti polisi mara moja kila mwezi.

Tags: DPPmashitakaMwandishitelevisheniuhainiWafutiwaWatatuWengine
TNC

TNC

Next Post

Uongozi wa kanisa wadai kuwepo uharibifu na upotevu wa mali

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company