Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Watano wafariki, mmoja ajeruhiwa kwenye ajali Arusha

by TNC
November 23, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Watu Watano Wafariki Katika Ajali ya Magari Mbuyuni, Monduli

Arusha – Watu watano wamefariki dunia na mmoja amejeruhiwa baada ya magari mawili kugongana katika maeneo ya Mbuyuni, Wilaya ya Monduli, mkoani Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo leo Jumapili Novemba 23, 2025, ajali hiyo imetokea saa saba mchana katika eneo hilo.

Kupitia taarifa hiyo, Kamanda Masejo amesema ajali imehusisha magari mawili ikiwemo basi la abiria aina ya Yutong lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Arusha.

Basi hilo la abiria liligongana na gari ndogo aina ya Mark X lililokuwa likitokea Arusha na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi mmoja.

Waliofariki katika ajali hiyo ni wanaume watatu na wanawake wawili, huku majeruhi akiwa ni mwanamke ambao wote walikuwa katika gari ndogo.

"Chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa na majeruhi amelazwa katika Hospitali ya Jeshi Monduli kwa ajili ya matibabu, huku miili ya marehemu ikiwa imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Makuyuni," ameeleza Kamanda Masejo kupitia taarifa hiyo.

Jeshi la Polisi Arusha linatoa wito kwa madereva na watumiaji wengine wa vyombo vya moto kuchukua tahadhari na kufuata sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani wakati wote waendeshapo vyombo vya moto ili kuepusha madhara ambayo yanaweza kutokea.

Uchunguzi wa ajali hiyo unaendelea ikiwa ni pamoja na utambuzi wa waliofariki.

Tags: AjaliajeruhiwaArushaKwenyeMmojaWafarikiWatano
TNC

TNC

Next Post

Suala la SUK bado, vigogo wajifungia kujadili

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company