Sunday, December 7, 2025
  • Login
No Result
View All Result
Instagram
TNC
  • Home
  • Home
No Result
View All Result
TNC
No Result
View All Result

Usafiri wa mwendokasi Dar wasitishwa kwa muda

by TNC
November 4, 2025
in Swahili
0
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Dar es Salaam. Serikali imetangaza kusitisha usafiri wa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam ambayo hutoa huduma kati ya Gerezani – Kimara na Gerezani – Mbagala.

Kusitishwa kwa huduma hiyo kunalenga kutoa nafasi ya kufanyika kwa tathmini ili kujua uharibifu uliofanyika wakati wa maandamano yaliyofanyika Jumatano ya Oktoba 29, 2025 jijini Dar es Salaam.

Katika maandamano hayo, waandamanaji waliharibu miundombinu hususan vituo vya mwendokasi vilivyopo barabara ya Morogoro kwa kuvunja vituo, mifumo ya ukataji tiketi na kuvichoma moto baadhi ya vituo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ametoa tangazo hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Chalamila amewataka watumiaji wa usafiri huo kutafuta njia mbadala za usafiri wakati ambao unafanyika utaratibu wa kurudisha hali kama ilivyokuwa awali.

"Tunasitisha mara moja usafiri huu ili kufanya tathmini ya kina ya uharibifu uliotokea kwani mifumo ya ukataji tiketi imeharibiwa jambo ambalo linahitaji muda ili kurudisha hali kama ilivyokuwa awali," amesema Chalamila.

Ameagiza Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra) kutoa vibali vya muda mfupi kwa mabasi ya kawaida ili yaweze kutoa huduma kwa njia ambazo zilikuwa zikitegemea mabasi ya mwendokasi.

Tags: DarkwamudaMwendokasiUsafiriwasitishwa
TNC

TNC

Next Post

Residents assured of peace, essential services

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Popular News

  • Zanzibar’s Leadership Advocates for Streamlined Tax System to Enhance Economic Growth

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanaohujumu miundombinu watachukuliwa hatua kali

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wasiwasi juu ya Uchochezi wa Makada katika Jimbo la Katavi

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • Wanawake Wanaonyonyesha Washauriwa Kula Milo Mitano Siku

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Category

  • English
  • Swahili

Socials

Instagram TikTok YouTube Facebook

About Us

TNC (Tanzania News Company) is the primary Source of News in English & Swahili in Tanzania

© 2025 TNC - Tanzania News Company

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In
No Result
View All Result
  • Home

© 2025 TNC - Tanzania News Company